Thursday, June 14, 2012

BAADHI YA VIFAA VYA KALE

mmoja wa waandishi wa

KASHIFA NZINTO KWA WATENDAJI BIHARAMULO


 Na
Magreth Chaba
Biharamulo
MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera  wametishia kumunganisha  mwenyekiti wao kwenye tuhuma zinazomkabili mweka hazina wa halmasauri hiyo baada ya kubaini kiasi cha sh.mill.101.8kutojulikana matumizi yake kufuatia kamati maalum iliyoiundwa februari 14,mwaka huu kuchunguza matumizi ya fedha za halmashauri hiyo.
Hatua hiyo ilikuja kufuatia mwenyekiti wa halmashauri hiyo,Apolinal Mugarura kuonyesha wazi wazi kumlinda mweka hazina huyo,Alexanda Bashaura na kuwabania madiwani kuchangia hoja za kamati hiyo zilizowasilishwa kwenye baraza hilo baada ya kamati yao kubaini utofauti wa zaidi ya sh.101.8 mill kwenye akaunti za halmashauri hiyo.
Akichangia hoja ya taarifa ya kamati teule ya madiwani,diwani viti maalumu Zayun Husein alisema,mbali na fedha hizo kutoonekana matumizi yake  mwenyekiti alionekana kumlinda mweka hazina na hivyo kudai kuwa kama ataendelea kumtetea na yeye watamuunganisha kwenye tuhuma hizo ili achunguzwe.
‘’Kama fedha hizo zinaonekana kuliwa na wewe mwenyekiti unaonekana unawatetea hawa watuhumiwa,tutakuunganisha na wewe kwenye tuhuma hizi za mweka hazina maana unaonekana kutubania sisi kuchangia hoja zetu,kwa hiyo na wewe uchunguzwe…hatuwezi kutetea upovu wa fedha hizi’’alisema Husein.
Kauli ya diwani huyo iliungwa mkono na madiwani wote bila kujali itikadi ya vyama vyao kwa maslahi ya kutetea fedha za umma kwa maendeleo ya miradi ya wananchi,ambapo mwenyekiti huyo alisema yuko tayari kuunganishwa kwenye tuhuma hizo na pia yuko wazi kuchunguzwa na kamati hiyo.
Akiwasilisha hoja za uchunguzi mwenyekiti wa  kamati ndogo iliyo undwa na baraza hilo Josephat Kayamba alisema,kutokana na uchunguzi wa kamati hiyo,kamati ilibaini kiasi hicho cha fedha baada ya kukuta kuna kasoro nyingi kwenye akaunti tano za halmashauri hiyo kati ya akaunti 32.
Kamati hiyo ya madiwani watano wakati wa uchunguzi wake ilikutana na kuwahoji watumishi watano wa halmashauri hiyo akiwemo mkurugenzi mtendaji Alhaji Zuberi Mbyana,mweka hazina,Mwanasheria ,mwenyekiti wao,mwaandishi wa vikao vya halmashauri  hiyo pamoja na meneja wa benki ya NMB Norbert Mwenga.
Kayamba alisema kamati ilichunguza kwa kina akaunti zote na kubaini tofauti kubwa katika akaunti tano za idara ya ardhi,tasaf,mamlaka ya maji ya mji wa Biharamulo,mfuko wa barabara na ukimwi na kugundua kuwepo kwa sh.101.8 kwenye benki kiasi ambacho kilitofautiana na taarifa iliyowasilishwa na mweka hazina kwenye kikao cha mwezi februari.
Taarifa hiyo ya kamati ya ilionyesha kuwa kiasi cha fedha iliyowasilishwa na mweka hazina mbele ya kikao cha  baraza la madiwani kilichopita kilionyesha kwenye akaunti hizo kuna sh.66.3 mill na kiasi halisi kilichoonekana kwenye akaunti baada ya uchunguzi kufanyika kulionekana kuwa na sh.168.1 na hivyo kamati kubaini utofauti wa sh.101.8 fedha  ambayo haijulikani matumizi yake.
Akijibu tuhuma hizo mweka hazina wa Halmashauri ya Wilaya hiyo Alexnda Bashaura amekiri kuwepo kwa tofauti ya fedha alizokuwa amezitolea taarifa ukilinganisha na taarifa ya uchunguzi wa wa kamati iliyo undwa na baraza hilo,na kudai kuwa taarifa hiyo imetofautiana kutokana na kwamba wakati anatoa taarifa hiyo kulikuwa fedha nyingine iliyokuwa imeingizwa kwenye akaunti hiyo kutoka hazina makao makuu fedha ambayo hakuwa na taarifa zake
Aidha Bashaura alisema kuhusu mchanganuo wa fedha hizo wakati akitoa taarifa hizo alidai kutumia vitabu vya malipo[cashebook]na si mizania ya banki[bankstatimate]zilizotumiwa na kamati ya madiwani baada ya kufuatilia taarifa hizo benki kwa kupitia akaunti zote za halmashauri hiyo.
Pia mweka hazina huyo alifafanua,kuwa taarifa ya vitabu vya fedha  vinatofautiana na ripoti za benki kutokana na kwamba fedha zimekuwa zikiingizwa kutoka hazina makao makuu Dar es Salaam bila taarifa na hivyo kupelekea kuwepo kwa mkanganyiko mkubwa wa hesabu za kifedha.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Alhaji Zuberi Mbyana ameiomba ofisi ya katibu tawala mkoa Kagera kuunda tume ya uchunguzi wa akaunti hizo ili waweze kuondoa utata na mkanganyiko wa matumizi ya fedha hizo.
Hata hivyo madiwani hao wameiagiza tume hiyo itakayo undwa na mkoa kuchunguza kwa kina akaunti hizo ikiwa ni pamoja na kuonyesha muda na siku wa kuingia kwa fedha hizo ili waweze kubaini kama kuna ubadhirifu juu ya fedha hizo.
                                              MWISHO

MADIWANI BIHARAMULO WALITUHUMU JESHI LA POLISI



 Na
 Magreth Chaba

Biharamulo

MADIWANI wa halmashauri ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera wamelituhumu jeshi la polisi wilayani humo kujihusisha na uharibifu wa mazingira baada ya kufumbia macho vitendo vya uvushwaji wa mkaa na magogo ya miti(Mbilimbi) kinyume cha sheria,ambapo mazao hayo husafirishwa na watu wanaosadikiwa wahamiaji haramu wa nje ya nchi na kuyapeleka nchini Rwanda.
 
Askari waliotuhumiwa ni wa kituo kidogo cha Nyakanazi wilayani humo ambapo wanadaiwa kushirikiana na wavunaji haramu wa raslimali ya misitu kutoka nchini Rwanda ambao huvusha mazao hayo kwa njia ya malori kupitia kizuizi kilichopo kwenye kituo hicho cha polisi licha ya kujua wazi kuwa kufanya hivyo ni kuhujumu uchumi wa taifa.
 
Hatua hiyo imekuja baada ya diwani wa kata ya Kalenge Gabriel Kakulu kutaka kujua chanzo cha uharibifu mkubwa wa misitu katika msitu wa hifadhi ya taifa wa Biharamulo upande wa kata ya Nyantakara ambapo eneo kubwa limeharibiwa vibaya baada ya wavamizi wa ndani na nje ya nchi kuingia ndani yake kinyume cha sheria na kujihusisha na ukataji miti ya kupasua mbao,uchomaji mkaa,kilimo na uchimbaji madini.
 
Kutokana na hali hiyo Kakulu alidai kutokuwa na imani na baadhi ya watendaji wa idara ya misitu waliopo kwenye kata hiyo pamoja na jeshi la polisi wilayani humo  kushindwa kudhibiti uvushwaji wa mazao hayo kinyume cha sheria licha ya mazao hayo kusafirishwa kupitia kizuizi cha polisi kilichopo jirani kabisa na kituo kidogo cha Nyakanazi ambapo yamekuwa yakipelekwa nchini Rwanda pasipo kutozwa ushuru hali inayopelekea halmashauri hiyo kupoteza mapato mengi kila kukicha.
 
Alisema halmashauri ya Biharamulo ilitarajia kukusanya shilingi Milioni tatu katika robo ya mwaka katika bejeti yake 2011/12 katika mapato yake ya ndani lakini kutokana na baadhi ya